• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

CHONYA AWATAKA MAAFISA WAANDIKISHAJI RUANGWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI NA UADILIFU

Posted on: May 14th, 2025

Afisa Uandikishaji Jimbo la Ruangwa, Ndugu Frank Fabian Chonya, amewataka Maafisa Waandikishaji Wasaidizi ngazi ya Kata kufanya kazi kwa weledi na uadilifu katika zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura awamu ya pili, akisisitiza kuwa Serikali imewaamini kutokana na uwezo na ujuzi walionao.


Chonya ameyasema hayo leo, Mei 14, 2025, wakati akifungua rasmi mafunzo ya Uboreshaji wa Daftari hilo awamu ya pili utakaoanza tarehe 16 Mei, 2025 hadi 22 Mei, 2025, mafunzo hayo yamefanyika katika bwalo la Shule ya Sekondari ya Wasichana Ruangwa, yakihusisha Maafisa Waandikishaji kutoka kata zote za Wilaya ya Ruangwa.


Aidha, amesisitiza kuwa uteuzi wa maafisa hao si jambo la kawaida bali ni dhamana ya kitaifa inayopaswa kutekelezwa kwa bidii na uadilifu wa hali ya juu. 

“Ni heshima kubwa kuaminiwa na kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, kumbukeni hii ni dhamana ya kitaifa, zingatieni maadili na mwongozo wa Tume.” amesema Chonya. 

Pamoja na hayo, amewakumbusha washiriki kuhakikisha wanashirikiana kikamilifu na Maafisa waandikishaji wa ngazi ya Kata na kuzingatia maadili ya kazi ili kuhakikisha kila hatua ya uandikishaji inafanyika kwa mujibu wa mwongozo wa Tume. Amesisitiza kuwa ushirikiano na uwajibikaji ni nguzo muhimu katika kufanikisha zoezi hilo.


Kwa upande mwingine, ameeleza kuwa ni muhimu kwa vyama vya siasa kupeleka mawakala wao katika vituo vya uandikishaji ili kuongeza uwazi na uaminifu wa mchakato huo, ingawa aliwakumbusha kuwa mawakala hao hawapaswi kuingilia majukumu ya maafisa waandikishaji. Ameonya kuwa nidhamu itazingatiwa kwa pande zote.

Zoezi hilo la kitaifa linatarajiwa kusaidia kuweka kumbukumbu sahihi ya wapiga kura na kuweka mazingira bora kwa ajili ya uchaguzi wa haki, huru na unaokubalika kwa pande zote, sambamba na kuimarisha demokrasia nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • WILAYA YA RUANGWA KUNUFAIKA NA MRADI WA URASIMISHAJI MAKAZI HOLELA

    June 24, 2025
  • WATUMISHI LINDI WATAKIWA KUTUMIA FURSA YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA KUJIFUNZA

    June 23, 2025
  • DED RUANGWA AKABIDHI VIFAA VYA MICHEZO KWA TIMU YA RUANGWA VETERAN’S

    June 21, 2025
  • DC NGOMA AZINDUA UWANJA WA MICHEZO WA RUANGWA VETERANS SPORTS CLUB

    June 21, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa