• Anuani zetu |
    • Maswali na Majibu |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Ruangwa District Council
Ruangwa District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Uongozi wa Halmashauri
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Ardhi
      • Elimu Msingi
      • Afya
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Fedha na Biashara
      • Elimu Sekondari
      • Mipango na Ufuatiliaji
      • Usafi na Mazingira
      • Kata
    • Vitengo
      • Mkaguzi wa Ndani
      • Ugavi
      • Nyuki
      • Sheria
      • Uchaguzi
      • Tehama
    • Kata
      • Nandagala
      • Mbekenyera
      • Likunja
      • Mnacho
        • Nangumbu
      • Malolo
      • Nachingwea
      • Ruangwa
      • Makanjiro
      • Mbwemkuru
      • Narungombe
      • Nangumbu
      • Luchelegwa
      • Chinongwa
      • Mandawa
      • Chunyu
      • Matambarale
      • Nkowe
      • Nambilanje
      • Nanganga
      • Namichiga
      • Mandarawe
      • Chibula
      • Chienjele
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Madini
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
  • Madiwani
    • Orodha ya Wah. Madiwani
    • Kamati za Kudumu
    • Ratiba
  • Mradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi ya Afya
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu
  • Kituo cha Habari
    • Videos
    • Hutuba
    • Albamu ya Picha
    • Habari
    • Tukio
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari

AIRTEL YAKABIDHI VIFAA VYA INTANETI KWA SHULE 23 RUANGWA

Posted on: August 20th, 2025

Kampuni ya simu za mkononi Airtel Tanzania, kwa kushirikiana na Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) na UNICEF, imekabidhi vifaa vya intaneti aina ya router kwa shule 23 za sekondari wilayani Ruangwa, mkoani Lindi, ikiwa ni hatua muhimu ya kuimarisha elimu kidijitali nchini.


Makabidhiano hayo yamefanyika leo Agosti 20, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, yakihusisha shule mbalimbali zikiwemo Chienjere, Chinongwe, Chunyu, Hawa Mchopa, Kitandi, Mandawa, Ruangwa, Kassim Majaliwa, Likunja, Nkowe, Mnacho, Nambawala, Mbekenyera, Mbwemkuru, Narungombe, Michenga, Mandarawe, Liuguru, Lucas Maria, Namichiga, Mary Majaliwa, Ruangwa Wasichana pamoja na Samia Suluhu Hassan.


Kupitia vifaa hivyo, walimu na wanafunzi sasa watapata nafasi ya kufikia moja kwa moja maktaba mtandao ya TET na jukwaa la Shule Direct, hatua inayotarajiwa kuinua viwango vya ufundishaji na ujifunzaji kwa kutumia teknolojia ya kisasa.

Aidha, walimu wa TEHAMA na wakuu wa shule wamepatiwa mafunzo maalum ya matumizi ya vifaa hivyo kutoka kwa Mwalimu wa Airtel Smart Wasomi, Harrison Isdory, ili kuhakikisha vinatumika kwa ufanisi katika kuongeza uelewa wa wanafunzi.


Akizungumza katika tukio hilo, Meneja wa Airtel Mkoa wa Lindi, Salehe Saphy, alisema kampuni hiyo itaendelea kushirikiana na Serikali na wadau wa elimu kuhakikisha kila mwanafunzi nchini anapata fursa ya kujifunza kwa njia ya kidijitali bila malipo.


Kwa upande wake, Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Lindi, Mwl. Kurwa James, aliwataka walimu kuhakikisha vifaa hivyo vinatumika kwa tija na kulindwa ili viwe na manufaa ya muda mrefu kwa maendeleo ya elimu.


Naye, Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Ruangwa, Mwl. Ernest Haule, aliishukuru Airtel, TET na UNICEF kwa mchango huo, huku akibainisha kuwa hatua hiyo inaunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuboresha elimu nchini.

Matangazo

  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA November 08, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA WAHUDUMU WA AFYA 872 KWA NGAZI YA JAMII HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA July 09, 2024
  • TANGAZO LA AJIRA HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA August 01, 2024
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA RUANGWA 27 MEI 2025 May 27, 2025
  • Ona zote

Habari mpya

  • ZIMEBAKI SIKU 15 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 14, 2025
  • HERI YA SIKU YA KUMBUKUMBU YA KIFO CHA MWALIMU NYERERE

    October 14, 2025
  • ZIMESALIA SIKU 16 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 13, 2025
  • ZIMESALIA SIKU 18 KUELEKEA UCHAGUZI MKUU WA RAIS, WABUNGE NA MADIWANI

    October 11, 2025
  • Ona zote

Video

MAENDELEO YATAKUJA KWA KULIPA USHURU, TOZO NA ADA ZA HALMASHAURI. MWANANCHI LI0A KODI KWA MAENDELEO YETU
Video zaidi

Kurasa za Haraka

  • Mpango wa Bajeti 2017/2018(MTEF)
  • Watumishi Portal

Kurasa zinazofanana

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • BARAZA LA MITIHANI

Idadi ya Wasomaji Duniani

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

Anuani zetu

    Ruangwa

    Anuani ya Posta: S.L.P 51

    Simu ya Mkononi: 0732932312

    simu: 0732932312

    Barua pepe: ded@ruangwadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera za Usiri
    • Kanusho
    • Maswali na Majibu
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa